Chombezo : On My High Horses
Sehemu Ya Tano (5)
Aaliyah: maskini pole sana jamaaan
Gigi: embu njoo hospital basi tuongee
Aaliyah: nipo best rest remember?! Siwezi nitakuja na mume wangu
Gigi: we Aaliyah kumbe ndo ulivyo ee, hauna hata shukrani no wonder Mark alikuacha
Aaliyah: ndio maana na wewe ulimwuua mumeo stupeeeed kaa na mlemavu wako mwenyewe shenzy, simu ikakatwa!
Gigi ana hasira hana hata hali, akampandia hewani Mark
We mark, hunijui sikujui lakini nimekuta namba yako kwa Best friend amelazwa amepooza kuna pesa za matibabu zinahitajika maana sijaona kadi yake ya bima ya afya
Mark: uuuwi jaman Best Friend wangu, naja naja naja mamaa najaaa
Baada ya dk 20 Mark akadondokaaa akaenda kuskiliza nini kimetokea akaelezwa cha uongo
Oh kuna demu alikuwa anampenda kusikia kaolewa akapaniki akaanza kupumua hawezi ndio kuzimia kuja kushtuka dokta ananiambia amepooza sa sijui ndugu zake wala nini
Mark akampandia hewani mzee na Maza yake wakaja pale maza yake na Best friend analia kweli kweli baba mtu haelewi akaelezwa akauliza Gigi amtaje huyo demu
Gigi: hayupo tz anaishi Urusi na huyo bwanake harudi leo wala kesho ( kha! Gigi kwa uongo ni noma)
Baba wa best friend akachoka basi wakaendelea kuuguza
Gigi akampandia hewani Tausi we hawara ya Best friend, bwanako huku amepooza njoo okota mzoga wako akamtajia na room namba
Baada ya lisaa 1 Tausi akadondoka na dera kama kweli kumbe mshenz tu
Akajidai pale analia lia, Gigi anamwangalia tu shubabti mkubwa anamzoom tu na drama zake
Baadae akamfuata akawa anaongea na Tausi
Tausi: jaman imekuwaje wewe ni nani
Gigi: mimi dadake, cousin ya best friend, mamake na Best friend ni shangazi yangu, Tausi akakubali
Gigi akaelezea ule ule uongo wake hakosei Tausi akaamini
Basi Tausi akamsahau bwana wake, kila siku ndo kushinda pale na nene
Gigi akajitoa likizo kwa mwezi anakuja mara 4 tena j2 tu si unajua tena cousin sio kila siku lakini Tausi hapo kiiila siku yupo na mama Best friend
Baada ya miezi 3 Best friend akafungua macho, dokta akajaribu atembee akashindwa
Akalazwa tena mwezi wa 4, anapelekwa mazoezi, anarudishwa, mwezi wa 5... mwezi wa 6 .. mwezi wa 7... mwezi wa 8 uzuri Bima ya Afya inalipa!
Baada ya miezi 9 Aaliyah akawa anajiandaa kujifungua na wala hajawahi kwenda kumwona Best friend kabisaaa
Mwezi huo wa tisa na wiki 3 akajifungua watoto mapacha, wakike na kiume
Baba Bonge akafurahi sana, kha! Akawaita majina ya marehemu wazazi wake baba bonge, 9 kumi watoto alijifungulia pale pale alipolazwa Mark, wazazi wa Mark wakaenda kusabahi wajukuu,
Baadae Aaliyah akaomba uzazi akalelewe kwa wazazi wake sio kwa mumewe na Baba Bonge kijijini akakubali
Baada ya siku 4 wakatoka hospital maana Aaliyah alijifungua kawaidaa
Gigi akasikia kuwa Aaliyah amejifungua watoto mapacha hapa hapa hospital maana alikutana na wazazi wa Aaliyah wanapeleka msosi kwa aaliyah
Gigi: jamaaani mimi sijui chochote wala sijaambiwa kitu mbonaaa!
Gigi a
kampandia hewani aaliyah akiwa kwenye gari yake akakuta namba unayopiga haipoo
Gigi: mxiiiiuuu, akamfuata nyumbani kwa mumewe baba bonge akaambiwa haishi hapa tena wamehama nyumba, akauliza wapi mlinzi akamwabia sijui mimi
Gigi akaenda mpaka kwa mama Aaliyah akashangaa anakatazwa kuingia na mlinzi akajua tu ni Aaliyah na mahasira yake akaondoka kwenda kumtafuta Babu mlinzi akamkuta hayupo bado hajarudi bondeni dah akaona arudi tu kwake akapange tena mbinu mpya maana wapiganaji wake washafeli
Mama Bonge:
Naskia babako amepata watoto mapacha na huyo hawara yake aliemuoa
Bonge: eeeh! Makubwaaa mimi hata sijui! kazaa na nani
Mama bonge: kuna malaya mmoja anaitwa Aaliyah!
Bonge akachokaaaa! Mama unasemajeee?! Huku ananyonyesha mwanae Mark the 2nd
Mama bonge: nimekwambia anaitwa Aaliyah, vepee unamjua au?!
Bonge: namjua?!kwani mama wewe ushamsahau Aaliyah?!
Alikuwa bibi wa Mark ukawatenganisha
Mama Bonge: heeee?! unajua nimemuona mara 1 t
uu doh!
http://pseudepigraphas.blogspot.com/
Bonge: kweli Malipo ni hapa hapa Duniani! Mama Karma imekurudiaaaa?! uuuwi huku anacheka
Mama Bonge: sasa unacheka nini na wewe buana?!
Bonge: aaaah, pole mamangu, ahahahahaha yule ambae ulimwibia mume amekuibia wako?!
Makuuubwa kweli Mungu yupo, inakupasa ukatubu dhambi zako zote mapema maana huko mbele pabayaaa, tena baba baada ya kuwa na wajukuu anakuwa na watoto, uuuwiiii haya bwana bibi wa mapacha umekuwa
Mama Bonge: embu niache mimi, kwa sasa nipo single hata na mimi nikitaka kuzaa nitazaa vile vile!
Bonge: akawa anacheka tu huku anamnywesha mwanae maziwa kwa chuchu za chupaaa
Mama bonge akaondoka, akaenda kukaa chumbani kwake, mara simu ikaitaaa kupokea kumbe ni lawyer
Lawyer: mama za masiku
Mama bonge: salama baba
Lawyer: nilipata mzigo wako mama sasa nakukumbushia ile kesi mama ni mwezi ujao uwe tayar kupanda kizimbani na watu wako uwaandae
Pia itabidi wiki ujayo tuonane ili tuwekane sawa jinsi ya kujibu maswali ya mahakama na watu wako pia wanatakiwa waje niwapange wale mashahidi wako
Mama Bonge: sawa babangu asante sana kunikumbushaa simu ikakatwa
Mama bonge akaumizwa kichwa weeee, haelewi itakuwaje hana ushahidi wa kutosha kumweka Gigi mahala pake pa aibu na kwenye matesooo na kumshinda kesi alioifungua, maana mume ndo huyo kaondoka na kimada umri wa mwanae wa mwisho dah sasa nafanyaje maana hata huyu hawara wangu hana ushahidi wa kutosha
Akawa anawaza na kuwazua akaishia kulalaa
Asubuhi kukakucha Gigi akapigiwa simu na Lawyer wake
Lawyer: mama salama?!
Gigi: salama
Lawyer: sijakuskia
Muda mwanangu vepee! Unajua kuwa kesi yako yaanza kuskilizwa wiki ijayo?!
Kuna pesa za kunilipa natakiwa nionane na wewe ili tuweke sawa jinsi utakavyotoa ushahidi pia huu ushahidi wako una nguvu ila nahitaji kuona watetezi wako?!
Hii ndo kesi ya mwisho tupate hukumuu jitahidi uje unione wiki ijayo sawa?!
Gigi: dah baba asante sana kwa kunikumbushaaa! Nilishasahau asante sana, sawa naja wiki ijayo simu ikakatwaa
Dah afadhali kesi ianze maana nishaona Dunia chungu sasa, nani atanisaidia kesi maana sasa huyu babu mzee keshaingiwa na hurumaaa
Akampandia hewani babu mzee hapatikani dah hii ni noma, akaenda nyumbani kwake akamkuta hajarudi ulizia mlinzi akamwambia atarudi wiki ijayo
Ulizia namba ya simu ya bondeni akapewa akampandia hewani baba baba baba rudi tz haraka kesi mwezi ujao lazima tujipangee mimi huku mambo yameharibika kabisaaa hamna msaada nakutegemea wewe tu hapa tafadhali usiniangushee
Babu Mzee: sawa mwanangu nitakuja kabla ya kesi maana huku nishapata kimwana napeleka mahari wiki ijayo naoaaaa kwaiyo nivumilie nitarudi kabla ya kesi
Gigi akachokaaa anajutaaa kwanini alimwambia akaoeee akamjibu kwa unyonge sawa baba hamna neno.
Gigi akatafakariii anaona ushahidi hana na hivi Best Friend kawa zoba na Aaliyah kajifungua akajiona yupo pekeyake akachoka akarudi home kulala
Mchana huo mama bonge akaonekana Kanisani kwa akina Gigi, akaingia ndani ana appointment na Mama mchungaji
Kuingia ndani wakasalimiana hapo wee, wakakumbushiana kumbe ni ma best wa siku nyingii
Mama Bonge: sasa mami
Wangu nina kesi mahakamani nakuhitaji wewe na mumeo mnisaidie kunitetea
Kuna katoto kalikuwa kakwe changu lakn ndo ivyooo tenaaa, alipeleka kesi Mahakamani kunishitaki mimi nifungwee lakini sasa sina ushahidi tosha, akamwagia ubuyu weee
Mama Mchungaji: akachekaaaa wewe mama bonge acha basi kunitania, huyu Gigi unaemsema wewe ni Gigi wa hapa kanisani kwangu au?!
Mama Bonge: Gigi anasali kwako?! Makubwaa una picha nimwone?!
Mama mchungaji: sina ila kama una picha yake we nipe nitakwambia kama ndie au sio
Mama Bonge: akatoa picha ya mkwewe Gigi
Mama mchungaji: ah ndio huyu mkweo?!
Basi anasali hapa lkn mbona ni mke wa mtu, mume wake anaitwa Best friend wana hela sana wanatoa sana wanajitoa Kanisani, mume wake si mwanasheria
Mama bonge: heee! Gigi kaolewa?!
Iyo mpya na nani?!
Best friend?! Hili jina mbona kama sio geni kwangu!?
Embu ngoja akampigia mwanae Bonge eti unamjua mtu yeyote anaitwa best friend?
Bonge: si best yake na mume wangu Mark?!
Mama bonge: ah sawa nimemkumbuka, ivi huyu best friend alioa?!
Bonge: mmmh sijui ila sidhani mama, sijaskia hata kwa Mark ila nimeskia ameparalyse juzi kati hapa Mark alienda kumcheki hospital na kwao maana alisharuhusiwa siku si nyingi sasa sijui kama ameoa ngoja namwuliza Mark nakujibu, simu ikakatwa
Mama mchungaji: vepee tenaa kuna shida?!
Mama bonge: nimeshamjua huyo mume unaemwongelea basi kama wanasali hapa ni vizuri, ila huyo mumewe best friend naambiwa ame paralyse yupo kwa wazazi wake kwani hamjui
Mama mchungaji: hapana wewe ndo unaniambia wala sijaskia
Kabisa
Mama bonge: ndo ivyo mama ndo ivyoo! Sasa turudi kwangu... kwasababu unamjua huyu Gigi itakuwa poa sana kama utatoa ushahidi Mahakamani kuhusu yeye
Kuna kimeo nataka unisaidie kutoa ushahidi kuwa Gigi ni pretender hajaokoka na unamfahamu vizuri sana
Mama mchungaji: mama bonge hapana iyo ni dhambi kwa Mungu Muumba siwezi fanya ivyo
Mama bonge: tena utamwambia amekuja kuficha makucha yake kwasababu kuna kesi anayo mahakamani ni mtu mbaya na amekiri kwako kuwa amemuua mwanangu yule aliefariki
Mama mchungaji: hapana mama bonge hio mipaka mibaya sasa tunavukaaa
Mama Bonge: utaiambia hivyo iyo Mahakama la sivyo nakushitaki na utanilipa pesa zangu nyingi tu
Mama mchungaji: siwezi fanya ivyo na wala usinitishie maisha
Mama Bonge: wewe mama nadhani haunijui kabisa, mimi ni israel ninaetembea sijafaaaa, utanilipa fedha zangu zoooote nikikupeleka Mahakamani wewe kwa matendo mabaya yote ulionifanyia hili kanisa utalifunga shenzy kabisa, akaingiza mkono kwenye pocho yake akatoa picha za mama mchungaji amelala na mumewe (baba bonge) akamchana live nitakufunga na utanilipia fidia wewe ndio umesababisha mimi na mume wangu tumeacha,
Pia picha hizi za mumeo ametembea na kila mtu mpaka Gigi unaemwona malaika
Mama mchungaji akatoa machooo, kweli mama Bonge Mafiaaa mpaka picha za Gigi na mumewangu anazo, najua nilikuwa nahisi lakini hii ni tooo muuuch
Mama Bonge akatoa picha za mama mchungai na Best friend wakati wanapeana raha hapo Kanisani, hotelini, Mama Mchungaji akachokaaaaa! http://pseudepigraphas.blogspot.com/
Kweli nimemkubali mama Bonge Mafiaa
Mama Bonge: akatoa picha za mama Mchungaji na wanaume aliolala nao mtaani, aliolala nao pale kanisaaa wazee wa kanisaaa kha!
Aibuuu
Nikizipeleka hizi mahakamani kanisa lafungwaaaa sasa unasemaje?
Utatoa ushahidi kinyume na matendo ya Gigi au?!
Ni bora kumkosa mtu mmoja ili uokoe maelfu ya kanisa lako, hata mafarisayo walimtoa Yesu kuokoa kanisa zima
Mama mchungaji: kwaiyo mama bonge unajua Neno sasa sio?
Mama Bonge: usipofanya kama navyokwambia nitakuweka pabaya nimeshakwambia, mimi ni israel ninaetembea utaniona mwanga na mchungu Tz utahama kama hautalala hela na mumeo namchukua mimi
Mama mchungaji: mchukua hata sasa ndio maana umeachwa na mumeo shenz kabisa
Mama bonge: mimi sina cha ku loose, nina wajukuu 4, nina pesa na mali kibao, wewe una nini?!
Watoto wako wapo wanasomaaa tukifunga kanisa hao watoto wanakuwa machokoraaa hawataenda shule, tena nitakuweka pabaya, endelea kunitukana
Sasa kama nilivyokwambia, j5 wiki ijayo address hii ni ya lawyer wangu na simu yake nenda kamwone, tafuta evidence zooote za Gigi mbaya na nzuri mpelekee atakuelezea jinsi ya kufanya na kuongea Mahakamani
La sivyo huu mwezi utauona mchunguuu
Mama Bonge akaondoka akabamiza mlango
Mama mchungaji akabakia mdomo wazi ameduwaa hajui anafanyaje
Aaliyah buana mtu wa surprise, akamwibukia Best friend kwaooo, akawakuta wazazi wake akaongea nao fastaa akamwona mgonjwa
Best friend kumwona Aaliyah analia tuuu! Machozi yanamtokaa
Aaliyah: best friend jaman pole, nisamehe i did what i had to do nimekufumania sasa na Gigi you leave me no choice, wazazi wa Best friend walitoka nje hawakuelewa ni nini
Aaliyah akaongea weee akaongeaaa akaongeaaa Best friend anatoa machozi,
Aaliyah akamkumbatia amamchumu mashavuni akamchumu mdomoni, good bye Best friend get well soon akaondoka
Best friend: akatoa machozi pale wazazi wakaja wakampeti peti usijali Mungu yupo atakusaidia utapata mwengine,
Best friend akanyamaza akatulia kabisa, baada ya siku 3 Gigi anapigiwa simu mama Best friend analia, Best friend Amefariki
Gigi hakuelewa akadondoka kwa mamake Best friend maiti ipo mochwarii alilia Gigi jaman kama mtoto mdogo utadhani amemzaa best friend
Akamwuliza mama nini tena mbaya akaambiwa 3 days ago alikuja Aaliyah akaongea nae akawa anatoa machozi, baadae akaonekana kuchangamka lakini baada ya siku 3 akafa usingizini kapelekwa hospital dokta anasema ilikuwa stroke amewaza sana tukajua labda aaliyah kamweleza kibaya kumbe walaa ni maneno ya kawaida yule binti alimweleza kwanini aliolewa na huyo alieolewa nae, maana tuliskiliza maongezi kwa cctv camera yetu hakuna baya alilomwambia wala kumpa
Gigi akachokaaaa: akampandia hewani Aaliyah hapatikani, akaona ngoja wamalize msiba kwanza
Msiba ukakaa siku 3 watu kibaooo wakaja akina Mark akina Tausi wanalia hawaami i maskini Best friend kama utaniiii, hadi
Mama mchungaji wa kanisani nae kajaaaaa chezeiya fake lawyer, badae wakazika makaburi ya kinondoni, watu wakaondoka lakini Gigi hakuondoka, akabakia kwenye kaburi analia tu analia tu haelewi imekuwaje Best friend jamaaan umeondoka umetuacha na wazazi wako tunakutegemeaa kwanini lakini Best friend kwanini katukana weee alipomaliza hasira yake akaondoka kurudi nyumbani kwake Best friend hayuuuupoooooo teeeeenaaaa, SHOW IKAISHAAAAA
I Vacationed in Hell
Baada ya msiba na wiki ikapita maana Gigi aliomba udhuru kwa lawyer wake, akapata simu kwa Mama mchungaji asijue hili wala lile akaambiwa aende kanisani,
Gigi: mImi bado nipo kwenye wiki na msiba mume wangu hata 40 sijamaliza siwezi kabisa nipo kwa wazazi
Mama mchungaji: mama mimi sio type ya kuchezwa huyo marehemu sio bwanako wala nini, mmekuja kanisani kwangu kunizunguka na Mungu kawalaani ndio maana kamwondoa shenzi kabisa
Gigi: akabonyeza record kwenye simu yake, mama kwani tatizo nini tena mbona wanizidishia machungu jamaaa?
Mama mchungaji: unajua wajinga na washenzi kama wewe huwa siwapendi kabisa ukitaka uwe salama hapa Tz ujisalimishe kwa pilato mwenyewe
Gigi: mama nadhani haujanielewa mimi siji nipo kwenye 40 ya mume wangu mpaka miezi 2 ipite nitakuja kukuona otherwise njoo wewe si unapajua nyumbani?!
Njoo, kuja kuniona ni moja ya huduma pia
Mama mchungaji: akakata simu
Gigi: akawa anawaza kuna nini mbona maza leo kageuka mbogo?! Nikienda nita prove kuwa ni dhaifu nikikaa nitaonyesha uimara wangu na umakini lkn mama kuna maneno kaongea sijaelewa embu ngoja niwashe antena alizowekaga marehemu best friend
Kuja kufungua mama mamaa mama mama kumbe mama bonge alishaenda kumlisha tango pori, kamtishia mineno akawa anairekodi ile convo yoteeee, akashtuka na hivi best friend hayupo akaona vita anaicheza mwenyewee kesi yenyewe hii imebakia wiki 3 tuingie Mahakaman sasa afanyaje
Akamcheki babu mzee bado anakula raha akamtonya best kafariki babu mzee hajashtuka mimi nipo na mke wangu
Kurudi tena tz sahau huyu kimwana amenichanganya sana sana sana
Gigi: akaona isiwe shida huyu baba naona kaamua kunitelekeza
Basi nipe zile evidence basi za Vera mama bonge
Babu Mzee: haloo haloo halooo sikuskii unakatika haloooo simu ikakatwa
Gigi: huyu ananiletea michezo ya kizamani hajui mimi mwenyewe wa zamani ngoja nikamfanyie umafia kwake ataisoma namba
Jioni saa 12 nanusu akatia timu kama jambazi nyumbani kwa Babu Mzee mlinzi akawa amekaa akasubiri asinzie sinzie akaondoka, ikafika saa 3 akarudi kumkuta amejilaza kwenye kiti chake akamchoma sindano kwa nguvu paaa akaingiza maji akachomoa fasta,
Mlinzi kushituka anasikia kitu kimemchoma sana lkn hakionii, akasimama kuangalia mazingira shwaaari akarudi kukaa akajikunyata hapo inaenda 4 usiku mlinzi akazama usingizini
Gigi akaingia kama komando yoso akafunga gate vzuri sana
akaingia home kwa Babu mzee akaziua ua cctv camera toa kila kitu zima kila kitu, mpaka anamaliza ilo zoezi hapo saa 6 usiku
Akaingia bedroom yake akaanza pekua pekua na wewe pekua pekua kila kitu akakutana na ile cd aliokuwa anam blackmail mama bonge mpaka akakubali kutoa talaka, pekua kila kitu kipo safi on mama bonge's favor, pekua pekua nyumba nzima hajapata kitu akamind, saa 9 usiku akasema ngoja nilale kidogo, akashtuka saa 11 azana ya waislam akaondoka amemwacha mlinzi kazimaaa anauchapa kiroho mbaya sio kitoto
Akawa amekaa anatunga tu sheria akaona hii kesi akishindwa hatopata uhuru wake akaondoka akaenda zake mpaka kwa lawyer, akaskiliza kwanza lawyer vepe?
Lawyer akamwambia mama tupo pabaya kusanya taarifa zako zooote za ukweli haraka kesi imekaribiaaa
Gigi akaondoka kwa lawyer amechokaaa hapo kejambishwa jambishwa kuwa atashindwa kesi akarudi nyumbani kutafakari akakumbuka chalii yake aliomba kumsaidia mpaka mauti akajivisha kama bibi wa kizenji akadondoka zenji full mass nondo pemba moja
Akatua kwenye koroboi baya baya, akaingia katembea akatokea mpaka baharini, kha kweli Gigi kaamua maana kuna ka mwendo toka koroboini mpaka kwa huyo best yake.
Ni umbali kama toka Mwenge mpaka Morocco, ilo ni zoezi tosha..
Kufika anamkuta rafkiake amekaa anapunga upepo kifua wazi.
Akamwita Marioon
Marion: kageuka, Mungu waaangu Gigi my love umekuja?
Wakakumbatiana my Gigi umepotea sana
Gigi: nimefika rafiki
Marion: unaendeleaje, unaonekana mpweke sana vepee!?
Gigi: not good Marion hali mbaya sana na sijui kama nitaondoka nchini
Marion: nilikwambia my love, yule mama mafia, nilikwambia usishindane na mama wa kimachame atakuua, usinge feli kesi yako ungechukua hela alizotaka kukupa!
Gigi: lakini mauti ya Babangu inaniuma, sikuweza kuondoka kiboya boya kama mtu alieshindwa!, noo
Marion: basi nambie nini wataka
Gigi: kushinda kesi na kuondoka nchini vizuri, nataka nikakae Marekani nisirudi tenaaa
Marion: plan yako ipoje
Gigi: akamwelezea wee wakaingia kazini,
WAKATI HUO HUO...http://pseudepigraphas.blogspot.com/
Mama bonge akampandia hewani mamchungaji, mbona haujaja kwa lawyer
Mamchungaj: akakata simu
Mama bonge: ah hanijui ee, ngoja nimwonyeshe show zangu
Ikafika j2, mama mchungaj na mumewe wanajiandaa kutoka kuwahi ibada ya kwanza, dereva hayupo, simu hapatikani, wakaondoka kwenye gar kuwasha haiwaki, wakaenda kwenye gar ingine ikawaka, matairi 2 flat tire, dah kuangalia saa saa 1 kasoro 5 asbh, kumpigia simu mchgj msaidiz hapatikan, basi wakaona watembee mpaka kwenye taxi dk 20 wakapata kufika church saa 2 kamili asbh kuingia ndan wanamkuta dereva anasifu anaabudu wanashangaa, mchgj msaidiz nae buzy anaongoza ibada watu wanaomba
Ibada ikaisha wakamwita dereva vepe mbona haujatufuata
Dereva: nilipata sms ya mama mchungaji kuwa nisije mtakuja wenyewe, akawaonyesha.
Mamchungaj anashangaa mimi sijatuma jamaa, mumewe na dereva wanamshangaa, huyu vepe mzima kweli?
Mamchungaji anakomaa sijatuma sijatuma.
Wakamwacha, wakarudi nyumbani saa 10 jioni mlinzi hayupo alafu nyumba inawaka moto upande m1
Wakaita majirani wakabomoa geti bomoa mlango wakamwagia mchanga, maji mpaka wakaumaliza.. Wanashangaa tuu shetwain wa j2 vepee?
Wakalala ivo ivo, asbh wanapigiwa simu kanisa laungua mama,
tunazima hapa unashindikanika, mamchungaj kahaha anamwambia mumewe waende hawana gar iwakapigia taxi hapatikani, wanapiga kwa mtoa taarifa hapatikani, wakachukua taxi mpaka church kufika hamna cha moto wala nini, wakamwuliza muhusika aliepiga simu hamna hajapiga simu yangu ilikufa nina mwezi wa 3 sina simu, mamchungaj akaanza kushangaa, mumewe anamwuliza vepe mama unakuwa mgonjwa skuizi au?
Mamchungj anashangaa mimi sio mgonjwa nimesema kweli jamani, wakaamua wampumzishe nyumbani
Akalala siku ya 1 ya 2 mumewe anamfuata mke wangu kuna kesi inakuja tuisikize, wakaja waleta kesi mama m1 anamshtaki mama mchgj ametembea na mumewe akatoa picha zile zile alizoonyesha mama bonge.
Bamchungaji anashangaa mkewangu aibu gani mama mlalamikaji analia anatukana mimi nateseka kwa mumewangu we unakula raha nyama wee, mimi naondoka ila Mungu atalipa akaondoka.
Mamchungaji akamkumbuka mama bonge akajikausha, siku akawa anaenda sokoni na dereva kufika sokoni ananunua vitu akaja kichaa na fimbo akampiga kichwani mgongoni began usoni mama analia watu hawamsaidii wanamwangalia tu, bdae dereva anaona mbona makelele akafunga gari akaenda kumcheka bimkubwa anavuja damu kambeba hospital moja akalazwa.
Mumewe akaja kumsabahi akamwuliza hajibu, akaondoka, usiku saa 6 akaingia mama bonge, akawa anamshangaa ameingiaje, akamsalimia pale
Mama mchungaj: unafanya nini hapa? Nani kakuingiza muda huu?
Mama bonge: umenisoma sasa ee? Ndio ushanielewa au bado?
Mama mchungaj: mwuaji mkubwa
Mama bonge: hata sasa naweza chomoa mipira ukafa, usicheze na mimi
Mama mchungaj: jaribu uone nabonyeza emmergency
Mama bonge: bonyeza tuone kama inafanya kazi,
Mamchungaj akabonyeza pale hamna kitu
Mabonge: sasa nakuua hapa hapa, amua utanisaidia au la?
Mamchungaj: akanyamaza
Mabonge: amua, akatoa mkasi, nikate mpira niache?
Mamchungaji: go to hell
Mama bonge: i vacationed in there
Akakata mpira wa mamchungaj wa upumuaji , mamchungaj akawa anahaha kupumua
Mama bonge: i'll see u in hell moron,
Akamfunika na mto akawa anahangaika kupumua mpaka akakata roho, mama bonge akaondoka amemwacha mama mchungaji hayupo tenaaa
Asbh bamchungaj akapigiwa simu kuwa mamchungaj hatunae, amefariki usiku, alichomoa waya wa upumuaji maana tumecheki cctv zote hamna mtu alieingia ndani kumdhuru kabisaaa,
Poleni sana baba mchungaji sisi tumechunguza tumeona kuwa mkeo
amejiua kwa kudhamiria
Dah bamchungaj akalia wee kama mtoto mdogo, wakaja wazee wa Kanisa baada ya masaa 2 kumsabahi.
Siku ya mazishi mama bonge akaendaa, kama stranger makaburini kakaa mbaliii, anazoom na mpenz wake mpyaa wa miaka mingi
Msoma taarifa za marehemu anasoma: marehemu alianza ku behave ajabu ajabu these last few days, mara atuambie kanisa limeungua mara anatumia watu sms kuwa wasije kutuchukua mara katembea na mume wa mtu mke kaja kulalamika ila ktk uchunguzi tulidhan yule mana amemdhuru ila imeonekana yule mama tangu atoke pale nyumbani alirudi kijijini kuuguza mamake!
Akaenda sokoni akaanza kupigwa na kichaa hatukuelewa kuna nini, akafikishwa hospital kwa mahututi ya kupigwa ndipo hapo mama mchungaj akajiua akiwa hospital ICU
Watu msibani wanaangaliana, hawaelewi hili movie vepee?!
http://pseudepigraphas.blogspot.com/
TUONANE TAR 27 APRIL 2018 SAA 1 USIKU YA TANZANIA.
________________________________
D. The good, the bad and the evil
Msiba ukaisha mchgj akawa anaomboleza na nini, wakaja wamama, wajane, wamama senior bachelor, wadada toxic bachelor, wadada single, basi kila mtu na pole yake ushuzii
wale wamama wa mjini waliotembea na Mchungaji
wadada walioahidiwa ndoa,
yani ni balaa,
izo kumbatio sasa doh,
Ninauhakika Marehemu alikuwa anazunguka kwenye kaburi huko alipo akiona haya majanga! sio kwa ufuska ule,
Watoto wa marehemu wanashangaa mama kaondoka ametuachia matatizo, Maana shoo ya kutoa pole utadhani maonyesho ya ulimbwende,
Mavazi sasa na flirting ya kufa mtu, vimini, leggings, basi kila siku hakosi mwanamke amekuja kutoa pole kwa Mchungaji Mgane
Wengine kupika, kufua, kudeki na Pastor mwenyewe alivyo mzinzi kila mtu anamnong'oneza kivyake,
wewe unafaa kuwa mke, mara wewe utanifaa, mara mkewangu wife nakuona, basi kila mwanamke anavimba kichwa kivyake, jitihada za kufua mwenye hela walipeleka kwa dry cleaners, mara menu ya hotels inayoletwa ni hatari,
watoto wa marehemu wanaishi paradiso ndogo hahahaha
Basi pastor akapata mwaliko kwa mama m1 senior bachelor akamfanyie maombi nyumbani kwake kumbe anategwa!
Mgane Pastor asijue mitego ya ibilisi maana ye mwenyewe anakula na ibilisi sahani moja,
Akaenda, kufika maza akamwita chumbani, huku ndio napata mashambulizi Pastor akaenda kutoa huduna ya kiroho kaanza kuombea pale akiwa ktk kumaliza yule mama akatokeza uchi wa mnyama, Jesus! mgane Pastor anashangaa,
Mgane Pastor: jaman we mama mimi sipo ivo nafanya shughuli ya bwana
Senior Bachelor: usijali Pastor hata hii nayokupa ni huduma tosha,
Ni shukran ya pekee kwako,
Umenifukuzia mapepo ila ukanisahau kuniombea na mimi sasa unaonaje ukaja kunibatiza kimwili ili niishi vizuri unajua sijawahi kupata mguso wa mwanaume kwa miaka 20 sasa tangu niokoke na maisha yamekuwa magumu sana kwangu na ya shida
Mgane Pastor: akajibwida akambeba senior Bachelor wa watu, wakazama Honey Moon,
Pastor nae havumi lakini yumo jamaaan, mechi anaiweza
Senior Bachelor hakutaka usiku uishee alitaman mechi iendelee lakini ndo ivyo akawa anakazana kuwa kwenye ule wakati (live into that moment)
Huko Pemba:
Gigi akaonekana yupo na Marion wanapanga makuu,
Mesenja wa Marion akamletea ripot Marion akatikisa kichwaaa... akamwambia Gigi, mimi nilikwambia kuwa huyu mama ni muuaji kabisa
Angalia amemuua Mama Mchungaj wa pale kanisani kwako, angalia hizi picha za msiba walikuwa wanazika makaburini, angalia za kuaga
Gigi: MUNGU WAAANGUU, sasa tunafanyaje
Wiki zenyewe zimebakia 2 tu mimi mbona nachoka zaidi jamaa sasa tunafanyaje?!
Marion: lazima tumjambishe jambishe lazima nitume vijana wangu wakafanya kazi ya kumchunguza tujue nani yupo juu yake tumpindue
Asbh kukakucha vijana wa Marion wakaingia Dar es salaam, wakapiga usnitch wanamzoom Mama Bonge anajiachiia kweli kweli mpaka anaenda kwa uyo bwana ake wa miaka mingi
Wakamzoom Bonge wakajua anaonana na matusi
Wakapeleka ripot ndani ya siku 2 badala ya 3, wakaambiwa warudi kwa Mchungaji, kwenda kumcheki Mchungaji anahama nyumba hadi nyumba
Gigi akamwambia Marion kuwa ana mzee wake m1 hamsomi somi anahisi anampendelea Mama Bonge na mimi nipo pekeyangu yupo huko bondeni
Marion: kwaiyo unataka tumfanyaje sasa huyu Mzee
Gigi: mpige jamba jamba mpaka aje aungane na mimi staki ujinga ajue mimi ndio Gigi the great na atoe ushirikiano mpaka nishinde kesi
Marion akatuma vijana wake 3 bondeni Africa Kusini kwenda kumrejesha Babu mzee wakatua bondeni, kumsaka babu mzee mwenyewe anakula kula raha hamna cha mke wala nini?
Wakampa jamba jamba wakakamata mishangigi ya kizulu ikamfilisi wakamwibia passport babu mzee wakamwitia na polisi akarudishwa Dar hana hata hela kufika Airport ana buku akapanda daladala mpaka kwake Bunju hakufunguliwa na mlinzi kuangalia nyumba shaghala baghala,
Hamna cha msosi, simu hana dah alichoka sana
Akakaa siku 3 njaa kali akaenda dukani kwa Mangi anaomba simu akampigia angalau Gigi, Mangi akampaa!
Babu Mzee: Mama salama nimesharudi Dar vp waendeleaje
Gigi: vibaya sana nipo tu sina hata 100
http://pseudepigraphas.blogspot.com/
Na ile kesi ni wiki 2 zijazooo basi nimeona nishindwe tu
Babu mzee: hapana Gigi usikate tamaa nitakusaidia
Gigi: kivipi? alafu mimi sina hela hela zote nimepeleka kwa lawyer sina hata 100
Babu Mzee: basi mama uje tuyajenge hamna lililoharibika, njoo tafadhali
Gigi: kama unataka kunisaidia nenda kamwone lawyer wangu kesho mpe vithibiti (evidence) vyako vyote, vinginevyo potezea akamtumia amwani na sehemu anafanya kazi lawyer,
Babu Mzee hapo kachoka hela kabakiwa na 200, akaona auze kitu kwa jirani akapata elfu 20, akaenda kumwona lawyer akampa evidence akaondoka, lawyer akampigia Gigi akamweleza Gigi akacheka akamwacha Babu Mzee ashike adabu kidogo hapo kwake
Huko Pemba Gigi akawa mwenyeji, anazurura wee anawafanyia wazungu utalii mara alale na wazungu, basi balaa tupu,
Marion akampigia simu wewe kimwana upo wapi?! Gigi akamwelezea
Marion: njoo hapa nyumbani kuna dharura ya balaa
Gigi akakimbia kufika anaambiwa fungua hii sahani kufungua tobaa kichwa cha matusi
Anamwuliza Marion huyu nani?!
Marion: vijana wangu wamekuletea kichwa cha Matusi,
Hayupo tena, bado tunamsaka bwana wa Mama Bonge wa miaka Mingi
Matusi alikuwa Bwana wa Bonge ndio aliempa ujauzito wa Bonge, na team yake yote wameisha bado tunamalizia team ya mpenzi wa mama bonge, mpaka sasa 50% wameondoka bado 50%
Hii ngoma ngumu lakini itaisha kabla Kesi
Gigi akachokaa akahamaki hajui ashukuru au amtunuku Marion kimwili au!
Maana kazi za kuweka kichwa kwwenye sahani sio zake kabisa, akahisi ameingia choo cha kiume
Bonge akakamatwa na watu asiowajua, wakamfunga macho, mikono, miguu wakampiga weee afu wakamtupa kwenye shimo reeeefu Bonge akashtukaaaa kuangalia saa saa 11 asbh kumbe alikuwa anaota akainuka kumwangalia mtoto wake amelala shwari, mume hayupoo dah akachoka akawa amekaa tu kitandani anawaza na kuwazua hajui ndoto ina maana gan, akaamua kumpandia hewani Matusi hapatikani
Akampandia mfuasi wake hapatikani, akampigia his right hand man hapatikani mmmh asbh ikawa ngumu
Akaamua kujiandaa hata job hakwendaa akaenda kumcheki Matusi, kufika nyumbani mwake kufungua ni madamu kibaooo watu wamekufa kiroho mbayaaa, hapo saa 12 asbh, akasogea kuangalia akakutana na kichwa cha Matusi kimekatwa, chini kuna karatasi imeandikwa you are next
Akakimbia mpaka kurudi home saa 1 asbh, akamwelezea maza yake, maza akaanza kuingia na wasiwasi akasema ngoja nimwulize mtu, kumpandia hewan big poppa che hapatikani wala nene,
Akampandia hewan msaidizi wake akamwambia ametekwa nyara hata wao wanamtafuta ila wanahisi kafichwa mikoani mistuni, mama bonge akachokaaa, akiangalia imevakia wiki 1 kuitwa mahakamani,
Mama Bonge: hajakuachia mzigo wangu wowote kabla hajapatwa na majanga?!
Msaidizi: ndio hata sisi twashangaa hata zile evidence zote zimepotea hazipo nadhan wamezichukuaa wale waliomteka Big Poppa yani mama hapa tumechanganyikiwa hatuelewi
Mama Bonge: kwani nyie hamna maadui zenu ambao mnahisi labda wanachukiana na Big Poppa
Msaidizi: tunae, anaitwa Matusi, sasa tumeenda kumcheki
Tumekuta keshauawa na kichwa kakatwa chini kuna karatasi imeandikwa you are next tukaondoka tusijekutwa na polisi hapo
Mama bonge akakosa pozi sasa maana hajui cha kufanya hajui afanyaje yani ni sheedah akakata simu akaendelea kuonge ana Bonge wanapanga juu ya usalama wao kesi wiki ijayo usalama wao mbovu hawajui cha kufanya dah hii ngoma ngumu
Wakiww wanaendelea kuumiza kichwa Mama Bonge akamkumbuka yule baba aliekuwa anampigia simu anamwimbia ila kwa namba ya private no
Akaenda tigo na voda kuulizia hawana msaada akaenda polisi kulalamika wakamwambia hii namba mbona haipo hewan ila ilikuwa inamilikiwa na babu mmoja akamtajaaa mama bonge akamkumbuka, akauliza kama anaweza pata current no yake, polisi wakamsaidia, kuna lingine au unataka tumkamate?!
Mama bonge: ngoja kwanza nitarudi afande ngoja niongee nae kwanza alafu ntakupigia kama mwingie kazini au la mama bonge akaondoka kufika job kazi haziendi akamwibukia hewani yule babu mzee akapokea
Mama bonge: eh vepee baba za masiku?!
Babu Mzee: salama, nani mwenzangu?!
Mama bonge: me fulani bin fulan
Babu mzee akaganda kama sekunde 5 akamwuliza enhe unataka nini kwangu?!
Mama bonge: nataka tuongee, napenda nikurudishe kazini najua haukuondoka vizuri, tafadhali naomba tuongee
Babu mzee: wapi tuongee sasa?!
Mama bonge: naomba tukutane sehemu flan, leo saa 10 jioni
Babu Mzee: sina nauli mama labda unifadhili
Mama bonge: ntakurushia elfu 30 uchukue taxi hapo uje fasta sawa
Babu Mzee: sawa mama asante, simu ikakatwaaa
Babu Mzee akampandia hewani
Gigi, mama nimepigiwa simu na mama bonge anataka kuongea na mimi
Keshatuma na hela hapa naona imeingia anataka kunirudisha kazini, niende au?!
Gigi: ulienda atakumaliza, ichukue hio hela we panda boat njoo pemba fanya fasta kabla hajakuletea watu kukumaliza
Babu Mzee: sawa mama akakata simu, akawa anakusanya kila chake, aondoke,ila anatoka tu mapolisi hao
Babu mzee upo chini ya ulinzi kwa kosa la kutishia amani ya mama bonge
Babu wa watu kawekwa pingu polisi moja
Saa 8 mama bonge akatia timu polisi, kumcheki mfanya kazi wake wa zamani anamwuliza me nawewe tumekoseana nini na tumekosana wap mpaka kuniletea majambazi nyumbani kwangu
Babu Mzee: me sina jambazi niliemleta mbonaa, unanisingizia embu liambie jeshi la polisi ukweli mama acha kuniweka kwenye wakati mgumu... babu kajitetea pale na nene lakini wapi
Huko Pemba nako Gigi akawa amepata wasiwasi akamweleza Marion, kuhusu yule Babu mzee me nahisi kuna kitu kibaya kinaendelea pale
Marion akampandia hewani ofisa wake, vepee natmatuta mtu anaitwa flan flan,
Ofisa: tunae ameletwa leo anashtakiwa na mama mmoja kibopa
Marion: ana kosa gan na dhaman gan?!
Ofisa: ana koss la kutishia amani ya huyu mama na dhamana yake dau mil 5, huyu ataozea jela
Marion: nikitoa mil 5.5 unaweza mtoa?!
Ofisa: sawa hamba shida mkuu
Simu ikakatwa
Marion akatuma kijaja wake amalipia dhamana, saa 10 dhamana akapewa akaondoka kijana wa Marion na Mzee mpaka Pemba, babu mzee anashangaa kitu kama movie vile
Kufika Pemba anashangaa anapokelewa na Gigi, he mama upo huku?
Umefikaje?!
Gigi: long story usijali, ilimradi upo salama hamna neno! Wakaingia ndani kupiga story, usiku wakala, wakanywa, wakacheka, wakachezaa wakalala
Asbh kukakucha, mama bonge akaamkia polisi saa 4 asbh, kufika anaambiwa mtu wako ametoka kwa dhamana ya mil 5.5 na mtu asiejulikana katuma kijana wake akamtoaa
Sie tumepokea maana dhamana uliweka wewe sio sisi
Mama bonge akachokaaa, dah! Nani huyu mshenz anafanya hivi jamaa! Akachoka akaamua kukaa chini kabisa sakafuni, machozi yanamtoka, kichwa kinamwuuumaaa
Ukiona mtu mzima analia, ujue kuna jambooooo!
MWISHO

0 Comments:
Post a Comment